Stori:Imelda Mtema
KAWAIDA
mkubwa ndiyo humfunda mdogo lakini mambo yalikwenda kinyume kwa
mwigizaji Yvonne-Cherry Ngatikwa ‘Monalisa’ ambaye alinaswa akimfunda
mama yake mzazi, Suzan Lewis ‘Natasha’.
Tukio
hilo lililopigwa chabo na paparazi wetu lilitokea hivi karibuni
nyumbani kwa shosti wa Natasha aitwaye Nuru, Tandika Maghorofani, Dar
wakati bi’mkubwa huyo alipokuwa akipewa somo (kufundwa) kabla ya
kuitumikia ndoa inayotarajiwa kufungwa ‘soon’.
Wakati baadhi ya
wafundaji tofauti wakiendelea kumfunda bi’mkubwa huyo mwenye umri wa
miaka 46, ghafla Monalisa aliomba na yeye amfunde mama yake ambapo
alianza kumshika mkono na kumpa ‘vipande’ vyake.
“Mh!
Sasa jamani mama kufundwa na mwanaye wapi kwa wapi? Ninavyojua mimi
mama ndiyo anaweza kumfunda mtoto sasa hii ya leo mpya,” alisikika
msanii mkubwa aliyeomba hifadhi ya jina gazetini.
Shughuli
hiyo iliyosheheni wageni waalikwa, ilitawaliwa na ngoma za asili kabla
msafara kuelekea nyumbani kwa Natasha, Yombo jijini Dar.
CHANZO: GPL
No comments:
Post a Comment