Breaking News

Sunday, December 9, 2012

MAELEZO YA TAMTHILIA MPYA YA SIRI YA MTUNGI


Familia kubwa inapokumbana na changamoto mbalimbali, baadhi ya wanafamilia  husambaratika na wengine huikabili kama sehemu ya mitihani ya maisha iliyowapitia.
Mchanganyiko mzuri wa wahusika wa Siri ya Mtungi, waliohusiana kwa damu au ndoa, au kwa mapenzi tu, unaunda jamii inayohamasishwa na penzi, lililoletwa na woga, ushirikina na usaliti, ikinyanyuliwa na ucheshi na furaha, na kupewa nguvu ya mshikamano wa ndani wa familia na urafiki. Ni hadithi ya mahusiano yaliyofaulu na yale yaliyopotea.
Ni hadithi ya mahusiano yaliyofaulu na yale yaliyopotea.
Kati ya mitaa yenye harakati nyingi ya Dar es Salaam na ile iliyo kimya ya Bagamoyo, tunapenya nyuma ya milango iliyofungwa mpaka kwenye maisha ya Cheche na mkewe Cheusi, binti wa kiongozi maarufu mwenye wake wengi, Mzee Kizito, pamoja na wahusika wengine kama Duma, mwana DJ;  Lulu- shangingi lililokubuhu; Farida- roho ya nyoka; Masharubu- mzee kikwekwe na wengine wengi.  
Cheche anapozawadiwa studio ya biashara na marehemu Habibu, mpigapicha wa Kiguru, anajikuta kuwa yeye si mpiga picha pekee bali ni kama alama au kitovu cha kile watu wengine wanachokitaka kutoka katika maisha. Mahusiano yake yakaanza kumletea matatizo.
Ndani ya picha anazopiga watu mbalimbali, au familia na marafiki, Cheche hukamata hisia mbalimbali za wanajamii zikionyesha matumaini, ndoto na matatizo ya kibinafsi.
Usikose kuangalia tathmilia hii saa 3:30 usiku kila Jumapili kwenye ITV, na saa 3:30 usiku kila Jumatano kwenye EATV!

No comments:

Designed By VungTauZ.Com