Breaking News

Monday, March 16, 2015

MOTO WAUNGUZA BWENI LA MABIBO HOSTEL JIJINI DAR

Wanafunzi wakijaribu kuokoa baadhi ya mali kutoka katika bweni la Block B kwenye hosteli ya Mabibo, Dar.
Moto ukiunguza bweni hilo.
Moshi mkali ukifuka kutoka katika bweni la Block B linaloendelea kuungua hivi sasa.
Wanafunzi wakishuhudia moto huo ukiendelea kuunguza bweni la Block B.
...wakitaharuki kutokea kwa moto huo.
....moto ukiendelea kuunguza bweni hilo.
Gari la zimamoto likiwasili eneo la tukio japo kwa kuchelewa.
Wanafunzi wakiwa nje ya jengo lililoungua wakati wakitafakari pakwenda.
Sehemu ya paa la jengo hilo iliyoungua.
Baadhi ya vitu vilivyookolewa.
Wafanyakazi wa Tanesco wakiwasiri eneo la tukio kutoa msaada.
Baadhi ya wanafunzi wakitafuta pakujihifadhi baada ya janga hilo.
Wanafunzi wakijadiliana jinsi ya kufanya.


MOTO mkali umeunguza bweni la Block B la hosteli ya Mabibo jijini Dar es Salaam muda huu. Chanzo cha moto huo na bado hakijafahamika.
Baadhi ya wanafunzi wanafanya jitihada za kuokoa mali zilizopo katika bweni hilo.

Moto mkubwa umezuka sehemu ya bweni la wanawake katika hosteli ya Chuo KiKuu cha Dar es Salaam lililopo Mabibo jijini Dar leo asubuhi na kusababisha vitu kadhaa kuungua pamoja na upotevu wa mali.
Katika tukio hilo wanafunzi wawili wamekimbizwa hospitali baada ya kuumia katika purukushani za kujiokoa ambapo mmoja alijirusha kutoka ghorofa ya pili ulipoanzia moto huo na mwingine aliumia kwenye mkanyagano wakati wa kujiokoa.
Chanzo: GLP


No comments:

Designed By VungTauZ.Com