Wanafunzi wakijaribu kuokoa baadhi ya mali kutoka katika bweni la Block B kwenye hosteli ya Mabibo, Dar.Baadhi ya wanafunzi wanafanya jitihada za kuokoa mali zilizopo katika bweni hilo.
Moto mkubwa umezuka sehemu ya bweni la wanawake katika hosteli ya Chuo KiKuu cha Dar es Salaam lililopo Mabibo jijini Dar leo asubuhi na kusababisha vitu kadhaa kuungua pamoja na upotevu wa mali.
Katika tukio hilo wanafunzi wawili wamekimbizwa hospitali baada ya kuumia katika purukushani za kujiokoa ambapo mmoja alijirusha kutoka ghorofa ya pili ulipoanzia moto huo na mwingine aliumia kwenye mkanyagano wakati wa kujiokoa.
Chanzo: GLP






No comments:
Post a Comment