Breaking News

Saturday, September 1, 2012

YANGA YAIFUNGA COAST UNION 2-1 MCHEZO WA KIRAFIKI


Kiungo wa Yanga, Haruna Niyonzima, akimtoka beki wa Coast Union, wakati wa mchezo wa kirafiki uliochezwa kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam, jioni ya leo.
Katika mchezo huo Yanga imeshinda 2-1, ambapo Coast Union ndiyo walikuwa wa kwanza kuandika bao katika kipindi cha kwanza, ambalo lilidumu hadi kumalizika kwa kipindi cha kwanza na kufanya timu hizo kwenda mapumzi huku Coast ikiwa mbele kwa bao 1-0.
Kipindi cha pili Yanga ilianza kucheza kwa presha na kasi iliyowachanganya zaidi Coast na kukosa mabao ya wazo na mipira mingine kigonga miamba.
Alikuwa ni Ally Shamte aliyepiga krosi matata iliyounganishwa moja kwa moja na beki wa Cost, Phillip Kaila, aliyeruka na kuuweka kimiani katika lango lake. bao la pili liliwekwa kimiani na Said Bahanuzi, bao lililodumu hadi kumalizika kwa kipute hicho

Jerry Tegete, akiruka tiktak na kukosa bao......

Mbuyu Twite, akijiandaa kumimina krosi mbele ya Nsa Job.

Joshua (kulia) akimdhibiti Nsa Job wa Coast.

Kavumbangu, akimiliki mpira mbele ya beki wa Coast.

Niyonzima, akikwepa kwanja la beki wa Coast Union.

CHANZO:www.sufianimafoto.blogspot.com

1 comment:

Unknown said...

yanga wametisha mbaya

Designed By VungTauZ.Com